Monday, June 16, 2008

MABADILIKO YA KIMAUMBILE NA MSONGO WA MAWAZO

Karibu mpenzi msomaji wa safu hii. Leo tutakaangalia jinsi ya kumsaidia mtoto, mambo yanayokupata, hali za kimaumbile na kihisia unazokabiliana nazo uwapo na msongo wa mawazo. Endelea nami pale ulipoishia wiki iliyopita.
UNAWEZA kumsaidia mtoto wako aweze kukabiliana na msongo wa mawazo kwa kuongea naye juu ya mambo yanayoweza kusababisha hali hiyo, ili aweze kuelewa. Ninaamini kuwa kwa pamoja, mnaweza mkapata baadhi ya njia zitakazoleta ufumbuzi kwake.
Baadhi ya majukumu anayokabiliana nayo mtoto, yanaweza kupunguzwa baada ya kutoka shuleni, pia ni vizuri kama atatumia muda wake mwingi kuzungumza na wazazi au walimu wake. Pia awe anafanya mazoezi ya viungo kama kwa kucheza michezo mbalimbali, au unaweza kupanga safari na kwenda.
Pia unaweza kumsaidia mtoto wako kwa kumwandalia kwenda kwenye warsha au mafunzo ambayo yatamwezesha kukabiliana na hali hiyo. Pia umpe uhuru aweze kujua muda atakaoweza kumwona daktari kwa ajili ya kuzungumza naye juu ya hali hiyo.
Kumbuka baadhi ya misongo ni hali ya kawaida, hivyo mwache mtoto wako aelewe kuwa si jambo la ajabu kuwa na hasira, kushtuka, upweke, au hali ya wasiwasi. Mwache ajue kuwa watu wengine nao wanapatwa hali kama hiyo siyo yeye peke yake.
Jinsi ya kushughulika na mtoto aliyepatwa na msongo wa mawazo Wakati watoto wanapatwa na shida katika kuzungumzia hali hiyo, itasaidia utakapozungumza na mtoto wako kuhusu mambo yako mwenyewe yanayokushughulisha. Hii itamsaidia kuona kuwa uko tayari kuzungumza naye kuhusu mambo yako unayokabiliana nayo, hali hiyo itamwezesha naye kujihisi utayari wa kuzungumza nawe jambo lolote linalomtatiza.
Kama mtoto wako ataendelea kuwa na hofu na kushindwa kuzungumza nawe kama mzazi wake, njia nyingine ya kumsaidia ni kumtafutia mshauri mwingine au daktari aliyebobea katika masuala hayo na kuzungumza naye.
Wazazi wengi wana uwezo wa kujua mawazo yanayowapata watoto wao, ikiwamo wakati wanaposoma na kukosa muda wa kupumzika. Mzazi kama utashindwa kukabiliana na hali inayomsumbua mtoto wako baada ya kufanya jitihada mbalimbali, mwone daktari wa mtoto wako, zungumza na washauri pamoja na walimu pale mtoto wako anaposoma. Baada ya kuzungumza nao, watakuwezesha kujua ukutane na mtaalamu gani ili aweze kumsaidia mtoto wako.
Tukiachana na jinsi ya kumsaidia mtoto wako ili aweze kukabiliana na msongo anaokuwa nao, pia kuna mabadiliko mbalimbali ya kimaumbile kwa mtu mwingine yeyote anapokuwa na msongo wa mawazo.
Mwitikio wa kimaumbile katika hisia kali uliumbwa ili kuweza kutuokoa katika siku zile ambazo watu waliishi katika mapango. Kwa mtu wa Zama za mawe, mwitikio wa kimaumbile uliojulikana kama ‘ruka au pigana’ ulimwandaa kwa ajili ya jambo lolote.
Mwitikio huo ulikuwa ni muhimu sana kwa matukio yaliyokuwa yakitokea mara chache pale alipokuwa akikimbizwa na wanyama wakali kama vile chui au alipokuwa akifanya mawindo kwa ajili ya chakula. Kwa sasa baada ya mamilioni ya miaka kuwa yamepita, bado mwitikio huo una visababisho sawa na vile vya wakati ule, lakini ni matokeo ya mibinyo tunayokumbana nayo katika maisha ya kila siku.
Ni kitu gani kinachotokea katika miili yetu tunapokuwa na msongo wa mawazo? Tunajikuta tunapatwa na shinikizo la damu, tunapumua kwa nguvu, masikio, macho na pua zetu zinakuwa na tahadhari mara zote. Mabadiliko haya ni matokeo ya kemikali zinazokwenda kwenye damu na kusababisha msongo kutokea.
Wakati unapoendelea kuwa na mawazo kwa muda mrefu, au yanapotokea mara kwa mara na kwa wakati mbaya inachangia kuwepo kwa hisia mbaya. Mwanadamu anapata onyo la kutoka kwenye ubongo ambalo linamwambia acha na upumzike.
Wakati tunapokataa kuchukua ushauri kutoka kwenye ubongo, inatuletea matatizo katika miili yetu. Hali hii inatofautiana kati ya mtu na mtu.
Ni jinsi gani mwonekano wako unavyoathirika?Baadhi ya watu wanaonekana kuishi katika maisha yenye mambo mengi ya kimitindo. Wengine wanaonekana kuwa na misongo kwa kiwango kidogo. Wote tuko kipekee kutokana na jinsi tunavyoshughulikia msongo. Kwa hakika msongo hautokani tu na yale yanayotusibu, lakini pia hutegemeana na jinsi tunavyofikiri.
Wanasaikolojia wanasema kuwa haiba tofauti hutenda tofauti na kukabiliana na msongo kwa njia tofauti. Kundi A la haiba ni wale ambao huwa na haraka katika mambo fulani, washindani na walio makini na hao ni wepesi wa kukumbwa na msongo. Kundi B la haiba ni wale ambao hawaonekani kujali sana, huchukulia kila jambo kama la kawaida tu hata kama ni kubwa kiasi gani. Hawa ni rahisi kukabiliana na msongo.
Kwa upande mwingine tuangalie tabia za kimaumbile katika msongo wa mawazo. Tabia hizo husababisha mtu kuogopa sana hadi kusababisha maumivu ya tumbo, kukosa hamu ya kula, kupatwa na maumivu ya kifua, kuharisha, kukondesha watoto, kukauka midomo, kutoka mkojo mara kwa mara, kuumwa kichwa, chakula kutokusagika vizuri tumboni, kukaza kwa misuli, kuwa na tahadhari ya mara kwa mara, mapigo ya moyo kupiga kwa nguvu bila kutegemea, kutopata usingizi, kutoka jasho jingi na kupatwa na maumivu yasiyoelezeka.
Tabia za kihisia unapokuwa na msongo wa mawazo. Mtu hujikuta kuwa na mabadiliko makubwa ambayo huchangia kuongezeka kwa wasiwasi, kero na kuwa na hali ya kutoeleweka. Hujikuta mambo madogo madogo yamkasirisha mara kwa mara na kumfanya ashindwe kuwa mstahamilivu.
Kwa mfano, ukweli ni kwamba watoto wanataka kucheza mchezo kwenye luninga, na wakati huo ndiyo kwanza umerudi nyumbani kutoka kazini, na unachotaka kukifanya ni kukaa na kunywa kinywaji chako huku ukiangalia luninga, kutokana na hali uliyonayo inakukusukuma kuwaondoa watoto wako na kukaa mwenyewe.
Pia kunakuwa na mabadiliko ya kutokuwa na hamu ya kula na wakati mwingine uzito kupungua. Baadhi ya watu wanakosa hamu ya kula, wengine wanakula kawaida. Uwezo wako wa kuendana na mazingira ya kazini na nyumbani unaweza kuwa tofauti, na unaweza kujikuta kuwa huwezi kulipa Ankara zinazokukabili lakini mambo huwa mabaya zaidi pale ambapo unakuta simu yako imekatwa kutokana na deni, ubongo wako unakuwa unawaza mambo tofauti na kukuongezea msongo. Unaanza kuvuta sigara au kunywa pombe au vyote kwa pamoja, hali ambayo unafikiri inakupunguzia mawazo, unapokuwa unakosa usingizi usiku.
Hali ya kihisia inayokupata unapokuwa na msongo wa mawazo. Unakuwa na hali ya kuhangaika au sononeko, unajikuta huwezi kufanya maamuzi, siku zote anakuwa na hofu au hali ya kutishika, hofu ya kutokea kuzimia au kuanguka, kusikia hali ya kupatwa na shinikizo la damu, kuhisi ubongo umekauka, kuhisi wasiwasi na kushindwa kupumzika, kuhisi kutoelewana na watu, kupatwa na msukumo wa kutaka kukimbia au kujificha, kuongeza majonzi pamoja na kuwa katika hali ya kutokutulia, na kutokuwa na uwezo wa kuwa makini na jambo.
Tukutane wiki ijayo.
lcyngowi@yahoo.com0713 331455/0733 331455

1 Maoni:

Ni wewe kuangalia kuanza mkopo biashara au kulipa
Hesabu za
Hiyo ni kwa nini tuko hapa kuwasaidia wenye
Unahitaji mkopo
kwa kiwango cha 3%
wasiliana nasi leo kupitia barua pepe:
joerichardloanfirm@gmail.com
Biblia inasema: "" Luke 11:10 Kila mtu ambaye anauliza
kupokea; atafutaye hupata; na kwamba
makofi mlango wazi "kwa kamwe kuondoka
wao miss nafasi kwa sababu Yesu ni
yule jana, leo na hata milele
zaidi.Tafadhali hizi ni nia mbaya na Mungu
wakihofia watu. Wewe ni ushauri wa kujaza na kurudi
.. Maelezo hapa chini name: __________
____________ Anuani yako: ____________________
Nchi yako: ____________________ wake
Kazi: Mikopo Kiasi __________________
Inahitajika: ______________ Mikopo Muda: ______
______________ Mapato ya kila mwezi: __________________
Kiini simu: ________________ Je,
kutumika kwa ajili ya mkopo kabla ya: ________________
haraka ndani na nje ya fedha dhiki, machafuko na
ugumu kuwasiliana RichardLoan Corporation
Leo email: joerichardloanfirm@gmail.com.you
Utapata mkopo wako bila kuchelewa kuwa Apply.and
heri

Twitter Facebook