Thursday, April 4, 2013

Hizi ndizo njia za kufanikiwa kibiashara


ILI ufanikiwe katika biashara yako inakubidi uwe na jitihada za ziada.
Kadiri mtu anavyoongeza jitihada katika usimamizi wa biashara yake, ndivyo anavyopata mafanikio.
Inapaswa kutumia jitihada za kiakili na kimwili.
Watu wengi huanza biashara baada ya kuchoka kutokana na kufanya kazi aliyoajiriwa kwa muda mrefu au kupata ‘presha’ kutoka kwa bosi wake ofisini.
Hivyo fikra kubwa aliyonayo ni kwamba katika biashara yake anakwenda kupumzika kwa kuwa ana wasaidizi, kazi yake itakuwa ni kusaini hundi tu.
Mwisho anakuja kushtukia hakuna biashara inayoendelea kwa kuwa hakuonesha jitihada tokea mwanzo.
Kumbuka kuwa kufanya biashara si jambo rahisi, linahitaji nidhamu ya hali ya juu katika utendaji kazi.
Uanzishwaji na ukuaji wa biashara unahitaji muda mwingi zaidi ya wengi wanavyodhani.
Hapo inabidi ufanye kazi muda mwingi, na kubakia na fedha kidogo za matumizi ya nyumbani, hadi pale biashara yako itakapoimarika.
Biashara inahitaji nidhamu ya hali ya juu, hata kama hakuna mtu anayekufuatilia au kukuonya pale unapokosea.
Inakupasa kuwa kwenye biashara yako kama ulivyojipangia ratiba yako ya kila siku.
Watu watakuwa wanakutafuta, pale wanapokuhitaji inabidi wajue unapatikana muda gani, unapokosekana unawavunja moyo wateja wako na kukosa fursa ambazo zingekupatia faida.
Pia inakubidi kutumia muda wa ziada na rasilimali zaidi endapo mauzo yako hayaendi vizuri.
Fanya soko au biashara yako ionekane kwa wateja wako.
Pia ni vizuri katika biashara unayoifanya, isihusishwe na familia yako. Hapa inamaanisha hata kama unafanya biashara, endapo mwanafamilia atahitaji kitu itambidi akinunue sio kuchukua bure.
Kuruhusu biashara yako iwe holela kwa familia, kutafanya ifilisike baada ya muda mfupi.
Ni vema kuweka muongozo mzuri kwa familia yako ili jambo hili liendelee.
Ushauri mwingine ni kwamba, ili biashara yako isonge mbele inakubidi uwe mvumilivu.
Ni kawaida biashara yoyote haiwezi kukua kwa siku moja. Inachukua muda kueleweka kwenye soko, kukubalika na wateja na kuweka mtandao safi.
Inabidi uwe imara katika malengo uliyojiwekea katika kipindi kigumu utakachokipitia.
Biashara nzuri ni kama miti mizuri inayochukua muda kukua. Lakini pale inapokuwa inastahimili kimbunga cha aina yoyote.
Na kama unaijenga biashara yako katika eneo lenye misukosuko ya kibiashara inakubidi uandae msingi imara unaohitaji uvumilivu.

1 Maoni:

The best casino bonus offers for players - GIOGaming
The best casino 샤오 미 먹튀 bonus offers for players · Play 뱃365 for 트 위치 룰렛 free · Play for free · Enjoy the best casino bonus offers · Stay safe · Enjoy the ibet789 sports betting asian handicap bonus experience. 텐벳

Twitter Facebook