Monday, June 16, 2008

FIKIRI UWE TAJIRI - 10

“HAKUNA mtu anayependa kuwa masikini,” maneno hayo yalisemwa na George Shaw. Naye Sophie Tucker anasema: “Nimeshakuwa tajiri, nimeshakuwa maskini, katika hali zote hizo maisha ya utajiri ni mazuri.
Kuna aina ya mafanikio mtu anayoyapata bila kutumia fedha. Pia kuna mafanikio mengine ili yapatikane inabidi uwe na fedha, inategemeana ni wapi unapoanzia ili kufikia malengo yako unayokusudia.
Fedha au utajiri ni jambo ambalo tunalipata kutokana na juhudi mbalimbali ambazo zinatufikisha kufikia malengo tuliyokusudia katika fikra zetu.Kwanza inapasa kujipanga na kujua jinsi gani utafanyia kazi fedha hizo ili kufikia malengo na matarajio yako.
Watu wengi wanasema kuwa pesa inaleta afya. Pia ukumbuke kuwa furaha ya kweli haipatikani kutokana na vitu ulivyonavyo, bali inapatikana kutokana na jinsi ulivyo, pamoja na uwezo wa kuweza kutumia malighafi uliyo nayo. Unaweza kuwa na fedha ili mradi kufurahia uhuru wa mwili na akili.
Mtu hawezi kuwa huru kama atakuwa anafanya kazi ya mfululizo kila siku na kupata kipato kidogo, endapo mtu huyo itamlazimu kulipa zaidi ya kile anachopata, mfano analipa gharama kubwa.
Katika mfululizo huu utaelewa njia ya kukufanya uwe huru kutoka kwenye vikwazo unavyokabiliana navyo na kufurahia maisha ya utajiri.
Njia ya kwanza ni muhimu kama unazika, mara moja , ile hali ya kuona kuwa pesa ni mbaya au haina umuhimu. Pesa siyo mbaya. Kama Biblia inavyosema, “kupenda pesa ni kubaya.” Ni kweli kuwa, pesa ni muhimu. Ni muhimu kama chakula na nguo kinavyohitajiwa kununuliwa, malazi, elimu na ankara unazotakiwa kulipia.
Pesa ni muhimu kwa yeyote anayeishi katika jamii ya waliostaarabika, na kufikiri kuwa si muhimu ni kujidanganya.
Kumbuka kuwa ni haki yako kuwa tajiri. Pesa ndiye dereva wetu mkubwa, inaongeza mtandao wako wa kuwa tajiri, inakuwezesha kupata utajiri ili uweze kuwasaidia wengine, na kumiliki fedha kwa faida itakusaidia wewe na familia yako kuwa na malengo ya mafanikio. Uwezekano wa kuwa na pesa unachangamsha akili yako kufikiria kufikia malengo uliyojiwekea.
Pia ni kawaida kuwa huwezi ukawa na furaha kama wewe ni maskini, na unahitaji kutokuwa maskini. Umaskini au kutokuwa tajiri ni aina ya maumivu yanayosababishwa na upumbavu wa mtu wa kuzijua kanuni katika akili yake ambazo zitamwongoza katika mafanikio.
Umaskini ni uchafu, unakufanya kutokuwa huru, pia unadhoofisha ujuzi ulio nao. Uko katika aina ya ugonjwa. Mtu maskini anajiona kama mfungwa, umaskini unawafanya wanaume na wanawake kupenda kunywa pombe, kula madawa ya kulevya na mara nyingine kujinyonga.
Umaskini unafanya kitu chenye thamani, kipaji, watoto wenye akili kugeuka na kufanya uhalifu. Unawafanya watu kufanya mambo ambayo hawajawahi kufikiria kama wangeyafanya.
Utajiri si pesa tu, bali hata amani uliyonayo ni utajiri. Amani katika akili yako ni jambo la thamani lenye mafanikio. Katika hali yoyote ile unapokuwa na amani, unakaribisha utajiri katika maisha yako. Pia inakusaidia kuishi maisha yako katika maeneo yako mwenyewe unayoyapenda. inakupatia amani katika kile unachochagua, ndiyo maana maisha yako kila siku yanakuwa ya kitajiri na yenye mafanikio.
Mtu mmoja alisema kuwa utajiri unakuja kwa mtu ambaye anaona umuhimu wa utajiri. Kama maelezo yaliyotangulia yalivyosema, huwezi kuwabeba wengine kuelekea mafanikio, lakini unaweza ukawaonyesha njia ya kila mmoja kujisaidia mwenyewe.
Je, ni kiasi gani cha pesa ambacho unataka kukimiliki? Chukua dakika chache na ujibu maswali yafuatayo.
Umepata nini kwa ajili ya kufanya biashara? Dunia imekufanyia nini kwa kile unachokifanya? Watu wangapi wanafanya kile unachokifanya? Utakapojibu maswali hayo, utajua ni kwanini baadhi ya watu wanakuwa na pesa nyingi zaidi ya wengine?
Kwa hiyo unatakiwa kuondoa mawazo yote uliyonayo juu ya umaskini, yanayokuzuia usisonge mbele kimaendeleo.
Umaskini si adui. Adui ni mtu ambaye wakati wote anaangalia si tu udhaifu alionao bali anauabudu pia.
Amekuwa akitumia nguvu zake kuwashawishi wenzake kuwa hakuna chochote wanachoweza kukifanya wakafanikiwa.
Ondoa kabisa mawazo yako potofu kuwa ni lazima uwe maskini. Kumbuka umaskini na mafanikio unatokana na akili yako. Kama utaamua kufuta mawazo ya umaskini, ni lazima uielekeze akili yako kwenye bahati njema, mafanikio na kufaulu. Kumbuka kuwa siri uliyoigundua ni sawa na shamba la almasi. Hii habari inaelezea siri kubwa ya maisha kwamba una shamba kubwa la almasi. Hizi almasi zilizopo zinajulikana kama jambo lenye kuwezekana na uwezo. Kuna uzuri mwingi wa vito vya thamani ndani yake, inatakiwa subira ili uweze kuchimba.
Ujuzi katika maisha yetu ya kila siku juu ya suala la kufikia malengo yenye mafanikio, unafundisha kuwa thamani ya sheria nyingi zinazosisitizwa katika kufikia malengo yako na kuwa tajri ni elimu.
Kwa kuwa elimu itakufanya kuwa mwelewa. Pili, kuwa mdadisi. Unapokuwa mdadisi uwapo shuleni, kazini au katika jumuiya. Jifunze kutoka kwa wengine, walimu wako, familia yako na rafiki zako. Kila mmoja ana kitu tofauti kwa ajili ya mwingine.
Tatu, amua ni nini unachohitaji nje ya maisha unayoyaishi. Kabiliana na changamoto mpya zinazokutatiza. Nne, kuwa tayari kupata faida katika nafasi zote zinazotokea kwako. Si tu kwa zile nafasi zinazogonga katika mlango wako. Kuwa wa tofauti.
Tano, usichukie. Chuki haizalishi. Wala haitakujengea chochote katika maisha yako. Na katika yote hayo, kuwa mkweli wa nafsi yako.
Kuwa mtu wa thamani na uligundue hilo. Jiamini. Kila siku uwe na maono mapya ambayo ni imara.
Fikiri uwe tajiri imefikia tamati.
Tukutane wiki ijayo kwa mada nyingine mpya.
lcyngowi@yahoo.com 0713 331455 0733 331455

0 Maoni:

Twitter Facebook