Monday, June 16, 2008

FIKIRI UWE TAJIRI - 9

ILI haiba iweze kuwa na mafaniko ni lazima idumu huku ikifanya kazi ya kutambulika ya Daniel James inataja ukweli kuwa haiba yenye mvuto si tu inaweza kufungua milango mingi bali inaweza pia kukusaidia ili uweze kuwa na kiwango cha juu cha ufanisi.
James alikulia katika nyakati za giza za huko Frorida nchini Marekani ambapo kulikuwa na ubaguzi wa rangi katika mji huo.
Miaka michache baadaye aliweza kushinda ubaguzi wakati akiwa katika jeshi baada ya kuwa Mmarekani mweusi wa pili kupandishwa cheo na kuwa Jenerali katika Jeshi la Anga la Marekani na kuwa mtu wa nne katika historia ya utumishi wa jeshi.
Utajiri na mafanikio ya James vilitokana na uwezo wa kuweza kutumia kikamilifu ushauri ambao mama yake alishirikiana naye wakati alipokuwa mtoto.
“Mama yangu alinifundisha misingi,” alikumbuka. “Upendo wa Mungu, upendo wa nchi na upendo wa mwanadamu. Na si kujaribu kuwa makini katika kukosoa kwamba umesahau kuangalia katika mazuri ambayo yako kwetu sisi wote.
“Kwa baadhi ya watu utahitajika kuchimba sana ili kuweza kupata sifa nzuri, lakini kila mtu anastahili pongezi na kuthaminiwa”.
Licha ya kukosekana haki ambako nimekumbana nako nilifahamau thamani ya kuthamini. Kama ningejazilizia sifa na kuthamini wafanyakazi wenzangu, nilijikuta kuwa nilikuwa na furaha ya kufanya hivyo.
James aliambatana na hekima hii maisha yake yote alikuwa na uwezo wa kuwafanya wale wote waliokuwa kando yake wajihisi kuwa ni maalumu kwa kuwatambua mmoja baada ya mwingine kwa kile kizuri walichofanya.
Alipuuzia ile dhana ya kwamba watu wengi unaokutana nao hujihisi kuwa ni bora zaidi yako kwa namna fulani. Aliamua kuugawa moyo wake kwa ajili ya wale waliokuwa wadogo kwake kwa kutambua umuhimu wao na mchango wao.
Aliwapa kile walichohitaji na mara nyingi ilikuwa ni kusifu kwa uwazi na uaminfu pamoja na kuthamini.
Ninaamini kuwa hutadharau mifano hii rahisi, lakini pengine zawadi yenye maana sana ambayo unaweza kuitoa kwa mtu mwingine nayo si nyingine isipokuwa kuthamini.
Kama bado unafikiri kuwa una mashaka juu ya dhana ya kwamba kusifu na kuthamini vina nguvu ya kimiujiza basi hebu jifunze katika mfano huu.
Kisa hiki kinaweza kuwa sawa na kilichopitwa na wakati lakini ujumbe wake unaonekana kuwa mbele ya wakati. Ilikuwa ni kawaida ya mtu mmoja mzee kukaa nje ya ukuta wa mji wa kale wa hapo alipokuwa akiishi akifanya kazi ya kuangalia wapita njia ambao walikuwa wakija kutoka upande mmoja na kuishia katika upande mwingine.
Kwa kawaida alipendelea kukaa katika kivuli akiwa amezungukwa na watoto akiwasimulia hadithi walizozipenda. Katika muda mwingi wa mchana wapita njia wengi wangependa kusimama hapo na kuzungumza naye.
Siku moja wakati wa majira ya joto mgeni moja alifika hapa na kuamua kusimama kwa muda ili aweze kuzungumzia na yule mzee ambaye kwa wakati wote huo alikuwa makini akiwasimulia hadithi marafiki zake watoto.
Mgeni yule alimsogelea mzee yule na kumuuliza: “Ninafikiria kuhamia katika mji wako huu je, unaweza kuniambia ni watu wa aina gani ambao wanaishi katika mji huu?”
Haraka mzee yule alisema, “Ni aina gani ya watu huishi katika mji ambao wewe unatoka?” yule mgeni alijibu kwa kusema: “Watu katika mji wangu si wakarimu, wanadanganya na kuiba na kusema uongo. Wanazungumza vibaya kila mmoja juu ya mwingine. Ninaondoka katika mji huo kwa sababu ya watu wasiofaa ambao wanaishi huko.”
Yule mzee alimwangalia mgeni yule kisha akasema: “Ninasikitika kukufahamisha kuwa utakutana na watu wa aina hiyo hiyo katika mji huu.” Na bila ya kusema neno lolote mgeni yule aligeuka nyuma na kuondoka zake na kumuacha yule mzee akiendelea na kuwasimulia watoto hadithi.
Muda mfupi baadaye mgeni mwingine akaja hadi katika lango la kuingilia katika mji huo, naye pia akasimama na kuanza kuongea. Akasema: “Mtu wangu mwema, ninahitaji kuingia mjini huu wa kwako je, unaweza kuniambia ni aina gani ya watu ambao wanaishi humo ndani?”
Yule mzee akauliza swali kama lile la mwanzo alilomuuliza yule mgeni wa mwanzo. “Ni aina gani ya watu ambao wanaishi katika mji ambao wewe unatoka?” Mgeni yule akajibu kwa kusema kuwa “Watu katika mji wangu ni wema sana. Wana urafiki na kila mtu wana upendo na wakati wote huwa wanaangalia uwezekano wa kutenda mambo mema kwa ajili ya watu wengine. Nilisikitika sana kuondoka katika mji ule kutokana na ukarimu na utu wema wa watu wake lakini hata hivyo kazi ninayoifanya inanilazimu kuondoka katika mji ule.”
Mzee yule alimshika mkono mgeni yule na kumwambia: “Utapata watu wa jinsi hiyo hapa. Karibu katika mji wetu.” Mgeni yule akatembea na kuingia kupitia katika lango la mji.
Watoto walikaa kimya. Baadaye mmoja wao alimsogelea mzee yule na kumuuliza “kwa nini babu hukuwaambia watu wale ukweli? Ulimwambia mmoja kuwa watu wetu walikuwa ni wabaya na mwingine kuwa watu wetu ni wazuri.” Mzee aliwaomba waketi ili aweze kuwaeleza.
“Nimewaambia ukweli,” alisema. “Mnaona, bila kujali kuwa mnakwenda wapi au mnafanya nini mtakuta aina ya watu mnaowataka katika jamii nyingine. Kama unataka watu wazuri mtawapata, lakini pia kama mnatafuta watu wabaya mtawapata pia bila shaka ndio mtakaopata. Kila mmoja wetu hapa ana sifa nzuri zaidi ya mbaya alizonazo. Siku zote jaribu kutafuta kilicho chema kutoka kwa watu wengine”.
Wakati fulani mtu mmoja alisema: “Ninajua furaha ni nini kwa sababu nimeshafanya kazi njema.” Mtu huyo alisema hivyo kwa sababu alifanya kazi nzuri na akapata kuthaminiwa na kusifiwa na wenzake kutokana na kile alichofanya.
Kutambua, kusifu na kupenda ni vitu vyenye kutia hamasa sana katika maisha. Tunapokumbana na vitu hivyo huwa tunaondoka katika eneo hilo ambalo tumekutana navyo tukiwa na furaha na kujihisi wenye thamani.
Kinyume chake ni kwamba tunapokosolewa huwa tunajihisi kuwa hatujitoshelezi na tusio na mwelekeo. Kwanini tunajisikia furaha pale tunaposifiwa? Ni kwa sababu kusifiwa maana yake ni utambulisho na uthibitisho wa thamani yetu.
Sifa huonyesha hutuambia kuwa tunaheshimika, tunahitajika na kuthaminiwa na hivyo kuonyesha kuwapo kwetu. Mara kadhaa huwa tunazuia sifa.
Wakati mwingine ni kwa sababu tunataka kuonekana kama wazalendo zaidi au wabinafsi zaidi. Lakini katika wakati mwingine hata hatuahangaiki kufanya juhudi.
Tunasahau kuwa kila mmoja hufurahia kutambauliwa, neno la kumsifia. Kusifia ni uthibitisho wa thamani yetu. Kusifu ni kukaririsha ushuhuda kuwa hisia zetu za ndani zimehalalishwa. Hutuambia kuwa tunahitajika.
Hivyo basi sifia wengine lakini pia usisahau kujisifia wewe mwenyewe pale unapostahili. Sifia maisha. Ni rahisi sana na jambo lenye kufurahisha kushiriki katika maisha ya mtu mwingine kwa kusema maneno machache lakini yenye kujenga.
Kusifu kwa dhati huhitaji nguvu kidogo sana na hufanyika kwa muda mfupi. Lakini matokeo yake huonekana baada ya muda mfupi lakini yakadumu kwa muda mrefu.
Tukutane wiki ijayo.
lcyngowi@yahoo.com 0713 331455, 0733 331455

0 Maoni:

Twitter Facebook