Friday, August 28, 2009

SAHAU MAUMIVU ULIYONAYO UPATE FURAHA

WIKI iliyopita tuliangalia jinsi ya kudhibiti hisia zetu ili tuendelee kuwa na furaha, imeonekana kuwa watu wengi wameshindwa kudhibiti hisia walizokuwa nazo na kujikuta wako katika hali ya kukata tamaa, pamoja na kuvunjika moyo. Katika mfululizo wa makala hizi za maisha yetu, nimedhamiria kukuletea kitu kipya kila Alhamisi. Leo tutaangalia jinsi inavyokupasa uyaachie mambo yanayokusumbua, ili uishi kwa furaha. Tutaangalia jinsi ya kuachana na mambo mbalimbali tunayokutana nayo katika maisha ili kuweza kupata amani na utulivu katika mioyo yetu. Kumbuka kuwa kama una tabia ya kuachana na ya maumivu na huzuni unayokabiliana nayo, utakuwa na maisha mazuri, lakini kinyume cha hapo, utaendelea kuwa mtu asiyekuwa na furaha siku zote. Na pia ufahamu kuwa, kila mmoja wetu hukabiliana na changamoto...

HALI YA KURIDHIKA INAONGEZA FURAHA

KATIKA mfululizo wa makala hizi za maisha yetu, nimedhamiria kukuletea kitu kipya, ambapo leo tutaangalia jinsi ya kudhibiti hisia zetu ili tuendelee kuwa na furaha. Watu ambao hawawezi kudhibiti hisia zao wanajikuta wako katika hali ya kukata tamaa na kuvunjika moyo. Lakini ukweli ni kwamba, inakupasa usikate tamaa mpaka kumwazia Mungu wako mambo mabaya, kutokana na wewe mwenyewe kushindwa kudhibiti hisia zako. Hivyo ni vema kuwa imara katika hisia zako, bila kujali kama unapitia hali ya milima na mabonde, ili kutimiza malengo yako uliyojiwekea, kinyume cha hapo, utaendelea kuwa mtu usiyesonga mbele kutokana na hali ambayo umeiruhusu, ilhali ungeweza kuidhibiti. Mfano mzuri ni kwa mtu aliyeelimika, kwa kuwa yuko tayari kufundishika, ambaye ni muelewa, hataabiki kwa kuonyesha kuwa...

IKUBALI HALI ULIYONAYO UPATE FURAHA

MSOMAJI, katika mfululizo wa makala hizi za maisha yetu, nimedhamiria kukuletea kitu kipya kila Alhamisi. Leo tutaangalia jinsi unavyoweza kupata furaha kwa kuikubali hali ya upungufu uliyonayo. Si rahisi kwa mtu yeyote kukubali hali ya uhitaji aliyonayo, lakini kufanya hivyo ni jambo la muhimu. Ni ukweli usiopingika kuwa, katika maeneo yote ya maisha tunayoyaishi, kanuni zake zinafanana. Na kwamba, unakuwa na furaha pale tu unapokubali hali ile ya upungufu uliyonayo, kwa kuwa hapo ndipo kwenye hitaji lako. Kama ni kweli kuwa kila mmoja wetu hajakamilika katika eneo fulani katika maisha, kwa nini basi unakuwa hauko tayari kuikubali hali hiyo? Wengi wetu tumekuwa hatuko tayari kukubali hali ya upungufu tuliyonayo, kwa kuhofia kuwa jamii inayotuzunguka itatucheka, kututenga ama kudhalilika....

TATUA TATIZO LINALOKUSUMBUA ILI UWE NA FURAHA

MSOMAJI wangu, katika mfululizo wa makala hizi za Maisha Yetu, nimedhamiria kukuletea kitu kipya kila Alhamisi. Leo tutaangalia jinsi ya kuwa na furaha katika maisha yetu ya kila siku. Hebu tuangalie mfano huu. Mwanamke mmoja alikuwa anahojiwa na mwandishi wa habari kwenye runinga na ghafla aliulizwa swali kama ‘anadhani ni watu gani siku hizi wana furaha’. Kwa taharuki bila utulivu, mwanamke yule alikurupuka na kujibu lile swali kuwa kila mtu ana matatizo mengi, akimaanisha kuwa hakuna mtu yeyote aliye na furaha. Hii inaonyesha dhahiri kuwa mwanamke yule kwa muda ule hakutarajiwa kuulizwa swali kama lile. Na aliulizwa bila kupewa nafasi ya kuwa na maandalizi. Na kwa muda huo, alikuwa ni mtu aliyejawa na mawazo. Lakini ukweli ni kwamba furaha huwa ipo tu, bila kujali kama mtu ana...

FEDHA HAZIWEZI KUKUPA FURAHA

KARIBU mpenzi msomaji katika safu hii ya Maisha Yetu, inayokujia kila Alhamisi, lengo likiwa ni kujifunza mambo mbalimbali tunayoyapitia. Leo tutaangalia mambo yanayoweza kukupa furaha katika maisha. Mara kwa mara waweza kufikiri kuwa kama ungekuwa na gari la aina fulani, nafsi yako ingeweza kufarijika. Kama ungeweza kumpata mtu mtakayeweza kuishi maisha ya ndoa katika raha na shida, ungekuwa na furaha, kama usingekuwa na hali ya msongo kutokana na ukosefu wa fedha, ungekuwa umejitosheleza. Ni kweli unaweza kuwaza mengi zaidi ya hayo kwamba kama ungeweza kufanya jambo fulani ama kuwa na magari, nyumba, dhahabu na vitu vingine vya thamani, ungeweza kuwa na furaha, lakini hicho pia siyo kipimo halisi cha kuhitimisha furaha yako. Sasa ni wapi ambako unaweza kuipata furaha, kama si kwenye...

HOFU HUSAIDIA KUEPUKA HATARI

KARIBU mpenzi msomaji katika safu ya Maisha Yetu inayokujia kila Alhamisi. Leo tutaangalia mbinu za kuwa jasiri katika uamuzi wako unaoufanya. Katika maisha yetu ya kila siku, tunaona kwamba mbinu za kuwa jasiri ni nzuri katika kukabiliana na hatari iliyo mbele yako. Lakini kwa wakati mwingine, mtu anapokuwa na hali ya hofu inamsaidia kutokana na sababu iliyopo. Ama tunaweza kusema unapokuwa na hofu, hali hiyo inakusaidia kwa kusudi maalumu. Ila kuna baadhi ya watu ambao hufikiri kuwa, si vizuri mtu kuwa na woga ama hofu. Lakini hii si kweli. Kwani hali ya hofu husaidia, ni ishara katika ubongo wako kwamba pale huenda pakawa na hatari. Zipo sababu nzuri zinazopasa kuwa na hofu, kwa kuwa hofu inayozungumza ndani yetu ni vema kuilinda mwenyewe. Kutokana na hofu unapokumbana na jambo,...

ZUNGUMZA NA MTOTO WAKO ASIPATWE NA MSONGO

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika siku nyingine ya leo, ambayo Mwenyezi Mungu ametujalia kuiona tena. Tunakwenda kuangalia hali ya msongo inayowakabili watoto pamoja na vijana wadogo. Ni ukweli usiopingika kuwa hali ya msongo inakuwepo katika hatua zote za maisha ya binadamu. Tunaona watoto wengi wenye umri wa miaka mitano na kuendelea, wamekuwa wakiona vitu mbalimbali katika nyumba zao ambavyo hufanywa na wazazi wao. Kwa mfano, kuna familia nyingine kila mara wazazi hugombana mbele ya watoto wao. Kama wazazi tuelewe, hali hiyo huleta hofu kwa mtoto na kuona kuwa baba au mama yake anaweza kumpiga wakati wowote. Wakati mwingine unakuta mzazi anaumwa na jino, maumivu anayoyapata anayaonyesha mbele ya mtoto wake, hali hiyo humjengea hofu. Kwani kuanzia hapo, inawezekana kabisa, mtoto...

WANAWAKE HUKABILIWA NA MSONGO KATIKA MAZINGIRA TOFAUTI

KARIBU mpenzi msomaji katika siku nyingine ambayo Mwenyezi Mungu ametujalia pumzi na uhai. Leo tutaangalia hali ya msongo inayowakabili wanawake. Wanawake wengi duniani, wamekuwa wakikabiliwa na changamoto nyingi, hali inayowafanya kupatwa na hofu, wasiwasi pamoja na kutojiamini. Changamoto nyingi huwakabili wanawake hao katika maeneo yao ya kazi, nyumbani na hata katika mazingira mbalimbali wanayokuwamo. Kwa mfano, kuna msemo usemao kuwa, binadamu wote ni sawa, lakini ukifuatilia msemo huo utaona kuwa, mara nyingi baadhi ya wanaume hawataki kukubaliana na msemo huo, kwa maelezo kuwa, wanawake hawana uwezo wa kufanya kazi zile ambazo wao huzifanya kwa umakini na uhodari. Kutokana na hali hiyo, ndiyo maana katika siku hizi za leo, wanawake nao wamekuwa wakihamasishana kugombea nafasi...

MSONGO KATIKA SEHEMU ZA KAZI (4)

NAWAKARIBISHA tena katika safu hii ya Maisha Yetu yenye lengo la kukufahamisha jinsi maisha yalivyo na yanavyopaswa kuwa. Leo tunaendelea na mada yetu ya msongo katika maeneo ya kazi ili uweze kujua jinsi ya kukabiliana na hali hiyo mara unapokutana nayo. Watafiti mbalimbali wamegundua kuwa, endapo bosi katika kampuni, atakuwa na hali ya msongo wa mawazo, ofisi, kampuni au shirika hilo litakuwa na mawasiliano mabaya. Naye mwanasaikolojia mmoja anayeshughulika na masuala ya viwandani amewahi kuelezea jinsi meneja mzuri anavyopaswa kuwa. Kwa maelezo ya mwanasaikolojia huyo, meneja mzuri anapaswa kuwa mshauri mzuri kwa wafanyakazi wake, ari ya kupenda kujituma, kupenda kufanya kazi na kushirikishana mambo mbalimbali na wafanyakazi wake. Kwa maelezo ya mwanasaikolojia huyo, endapo bosi...

MSONGO KATIKA SEHEMU ZA KAZI (3)

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika siku nyingine ambayo Mwenyezi Mungu ametujalia kuiona. Leo tutaendelea kuangalia mada kuhusu msongo katika sehemu za kazi. Wengi wetu tumekuwa tukikabiliana na hali ya msongo katika vipindi mbalimbali vya maisha, kuanzia kipindi cha utoto hadi uzee. Hali hiyo humpata mtu anayefanya kazi, mzazi katika kipindi cha kulea watoto wake na katika vipindi mbalimbali vya maisha. Ila humjia kila mmoja kwa jinsi yake. Mafanikio yetu katika maisha na thamani ya maisha, inategemea ni jinsi gani tunavyokabiliana na hali hiyo. Tunahitaji kuelewa msongo ni kitu gani na kujifunza jinsi ya kukabiliana na hali hiyo. Mtaalamu mmoja aliwahi kuelezea fani saba ambazo haziepukiki katika suala la msongo, ambazo ni fani ya ualimu, uuguzi, umeneja, ustawi wa jamii, udereva, ...

MSONGO KATIKA SEHEMU ZA KAZI

KWA mara nyingine nawakaribisha tena katika safu hii ya Maisha Yetu, inayokujia kila Alhamisi, lengo likiwa ni kuelimisha. Wiki iliyopita tulizungumzia kuhusu msongo katika maeneo ya kazi, tuliona sababu zinazosababisha mtu kupatwa na msongo katika eneo la kazi ni hofu, ongezeko la muda wa kazi, ilhali masilahi ni madogo na msisitizo wa kuongeza uzalishaji kazini wakati hakuna ongezeko la marupurupu yoyote. Leo ni mwendelezo wa makala ile na tutaangalia jinsi ya kuondoa hali hiyo, ambayo kwanza inakubidi ujijali wewe mwenyewe. Wakati msongo katika kazi yako unaingilia uwezo wako wa kufanya kazi, ni vema kujijali wewe mwenyewe, au kusimamia maisha yako mwenyewe, ni wakati wa kuchukua hatua. Wakati unapodhamiria kujali mahitaji yako, unakuwa na nguvu ya kushinda hali hiyo ya msongo....

ONYESHA UPENDO KWA RAFIKI, FAMILIA

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika safu hii ya Maisha Yetu. Leo tunaangalia jinsi unavyoweza kuonyesha zawadi ya upendo kwa watu, hata kama huna fedha. Kila mtu anapenda kupendwa, hivyo yakupasa kuwa na rafiki wa karibu atakayekushirikisha katika mambo mbalimbali anayokabiliana nayo. Kutokana na ukweli huo ni vema kuwa na rafiki mzuri na kuonyesha upendo wako kwake, kwa sababu wakati mwingine unajikuta hata familia yako inakuwa mbali nawe, ilhali katika kipindi hicho unahitaji mtu wa kuongea naye. Ni muhimu kuwa rafiki mzuri kwa sababu unajifunza ni jinsi gani ya kukutana na watu wapya na unajifunza kutokana na makosa yako. Tafuta watu unaopenda wawe rafiki zako, kwa kujitambulisha na kumwacha mwingine kukueleza juu ya mambo anayoyapendelea. Mwonyeshe mtu huyo kuwa unamwamini, mwache...

JIFUNZE KUSHUKURU

KARIBUNI wapenzi wasomaji wetu katika safu hii ya Maisha Yetu inayokujia kila alhamisi. Leo tutaangalia jinsi ya kutoa shukrani. Kila siku ni njema ya kukuwezesha wewe kutoa shukrani kwa vitu vyote ulivyonavyo katika maisha yako. Kuna baadhi ya watu, wamekuwa wakifikiri ni jambo gani la kuweza kulitolea shukrani. Wengi wenu wanaweza wakawa wamepoteza kazi au nyumba zao. Pengine umekabiliana na changamoto katika afya yako au uhusiano wako. Bila kujali hali uliyo nayo, ni vema ukawa mtu wa kushukuru kwa kuwa Mungu kwani ndiye anayejua mambo mema anayokuwazia kila siku. Kamwe sijawahi kukutana na yeyote ambaye hana kitu chochote cha kumfanya ashukuru. Inapokuwa unahisi kuwa huna jambo lolote la kulitolea shukrani, unakuwa unakosea kwa sababu ulimwengu hauwezi kukupa zaidi ya kile ulichonacho....

Pages 321234 »
Twitter Facebook