Wednesday, December 12, 2012

Jinsi ya kuepuka kupata hasara

BIASHARA yako inapokwenda mrama, ni vema kuweka tamko la kusitisha hasara uliyoipata, kwamba hauko tayari kukubali iendelee. Jitahidi kuweka mikakati zaidi ya kuiboresha na kuomba ushauri wa kimaendeleo kwa waliofanikiwa. Tumwangalie mfanyabiashara John Robert, aliyekuwa amepewa fedha na rafiki zake kiasi cha dola 200,000 za Kimarekani, ili kuwekeza katika soko la hisa. Baada ya kupewa fedha hizo na kuzifanyia biashara, Robert alifikiri kuwa angepata faida ambayo ingemfanya awe na maendeleo zaidi katika maisha yake, lakini kwa bahati mbaya ilikuwa kinyume na matarajio yake. Awali, alipoanza biashara hiyo alipata faida iliyomfanya asiwe mbunifu katika biashara yake, lakini matokeo yake ni kwamba baada ya muda mfupi alifilisika. Baada ya kufilisika, alipata hofu kutokana na fedha alizopewa...

Kwa nini wajasiriamali hukopa, hawafanikiwi? - 3

WIKI mbili zilizopita nilizungumzia kwanini wajasiriamali wengi na wafanyabiashara wa kati licha ya kukopa kwenye taasisi za fedha wanashindwa kufikia malengo waliyojiwekea. Baadhi ya wajasiriamali hao walitoa sababu katika safu hii ya Maisha Yetu inayowafanya wasisonge mbele katika shughuli wanazozifanya. Pamoja na sababu hizo zilizotolewa, bado elimu kwa wajasiriamali hao inahitajika kwa kiasi kikubwa. Inatakiwa wapate elimu kuhusu biashara wanazozifanya na kwamba endapo watapeta fedha wanatakiwa kuzitumia vipi. Ukweli ni kwamba kumpa mjasiriamali fedha tu, hapo unakuwa hujamsaidia. Cha msingi ni kumpa fedha hiyo pamoja na elimu ya jinsi ya kuboresha biashara anayoifanya. Wapo wajasiriamali waliofanikiwa kutokana na nidhamu ya fedha wanayoipata ikiwemo pia elimu kuhusu shughuli anayoifanya. Ni...

Kwa nini wajasiriamali hukopa, hawafanikiwi? - 2

WIKI iliyopita katika safu hii tuliangalia kwa kifupi ni kwanini wajasiriamali wengi na wafanyabiashara wa kati, pamoja na kukopa kwenye taasisi za fedha au benki wanashindwa kufikia malengo yao. Leo tutachapisha maoni mbalimbali ya wasomaji wa safu hii ambao wameyatoa katika kuelezea changamoto hiyo inayowakabili wajasiriamali. Mmojawapo wa wasomaji hao aliyejitambulisha kuwa ni Alexander kutoka Dar es Salaam, anasema tatizo kubwa kabisa ni wajasiriamali wengi wanakuwa hawana ndoto ya kufanya wanachotaka, hivyo wanapokopeshwa fedha hizo hushindwa kuendelea. Matokeo yake hujikuta wakitangatanga katika biashara nyingi kwa kuwa hawakujua wanataka kufanya nini. Msomaji mwingine kutoka Mwanza ambaye hakujitambulisha jina lake alisema kuwa, taasisi nyingi za fedha ama benki zimekuwa ni kikwazo...

Kwa nini wajasiriamali hukopo, hawafanikiwi? - 1

HAKUNA mtu asiyependa kufikia malengo yake aliyojiwekea kwa wakati. Mara zote wajasiriamali wadogo au wafanyabiashara wa kati wamekuwa wakitamani kupata mafanikio, lakini wanakabiliana na changamoto mbalimbali. Changamoto hizo ndizo zinazowafanya wasifikie ndoto zao za kuongeza biashara nyingine, ama kupanua biashara zao kwa muda maalumu. Jambo hili limekuwa ni kilio kwa wajasiriamali wengi ambao wamekuwa wakiomba mikopo katika taasisi mbalimbali za fedha au benki, lakini matokeo yake fedha yote huishia kulipa madeni hayo. Hivyo wanajikuta hawasongi mbele. Ninajua zipo sababu nyingi sana zinazowafanya wasisonge mbele, lakini leo tutaambiana kwa uchache. Zaidi nitapenda kujifunza kwa wajasiriamali wenyewe ambao nitapenda wanitumie maoni yao kupitia simu yangu ya mkononi ama e-mail yangu...

Ugumu wa maisha wawatatiza vijana 2

NAKUKARIBISHA katika safu hii ili kupata elimu juu ya maisha yetu ya kila siku. Wiki iliyopita nilizungumzia vijana wenye umri wa kujitegemea kuendelea kuishi na wazazi wao kutokana na ugumu wa maisha uliopo. Leo nitaendelea na mada hiyo huku nikizungumzia jinsi gani kijana anayekaa na wazazi wake anapaswa kufanya nini ili kuonesha kama amekomaa. Ili kuonesha kama umekomaa unapoishi na wazazi wako, onesha kuwa upo nao kwa muda tu, kwa kuwa una mpango wa kwenda kuishi katika eneo lako. Kabla ya kuondoka nyumbani kwa wazazi ni vizuri ukawaeleza ni lini unatarajia kuanza maisha ya kujitegemea. Kijana anapokuwa nyumbani kwa wazazi wake anazungukwa na maadili yaliyopo katika nyumba yao. Kwa mfano atapenda kuangaliwa kwa ukaribu na wazazi wake katika mahitaji yake. Lakini kama kijana huyo...

Ugumu wa Maisha wawatatiza vijana

NAMSHUKURU Mwenyezi Mungu kwa kuniwezesha kukutana nawe tena katika safu hii inayokujia kila Alhamisi. Katika miaka ya hivi karibuni vijana wengi wenye umri wa kujitegemea wamekuwa wakiishi na wazazi wao kwa kuogopa kupanga kutokana na changamoto mbalimbali zilizopo. Kuendelea kuishi na wazazi baada ya kuhitimu chuo, ni jambo linalorudisha nyuma fikra za kijana au anakuwa na mawazo ya kudumaa. Ukweli ni kwamba, vijana wa kiume wenye umri miaka 25 na 34 siku hizi wamekuwa wakirudi nyumbani kwa wazazi wao kwa ajili ya kuangalia video na michezo mbalimbali katika nyumba za wazazi wao. Vijana hao wamekuwa wakiukataa ukweli halisi kuwa wamekwishakuwa wakubwa na wanapaswa kujitegemea. Vijana wa aina hiyo wamekuwa wavivu, hawapendi kujishughulisha katika shughuli mbalimbali, wengi wao wakiwa...

Pages 321234 »
Twitter Facebook