KWA mara nyingine tena, ninapenda kuwakaribisha wasomaji wangu katika safu hii inayokujia kila alhamisi, ili uweze kuelimika kwa kupata mawazo mbalimbali.Leo tutaenda kuangalia njia mbadala za kufanya baada ya kukumbana na misukosuko mbalimbali kutoka kwa bosi, mkuu wa kitengo au mkurugenzi wako.Watu wengi wamekuwa wakivunjika moyo na wengine wao kuamua kuacha kazi eti kwa sababu bosi wake hampendi, lakini ikumbukwe kuwa hiyo siyo suluhu kwako kwani kuna hatua mbalimbali za kufuata kabla ya kuchukua uamuzi wako ulioukusudia.Je umeshoka? Umekata tamaa? Huna furaha? au Hupati hamasa katika kazi yako? Pia inawezekana kwamba mawasiliano yako na bosi wako yanakufanya uwe mnyonge, kwa kuwa ni mwonevu, mkatili na mkandamizaji. Anaingilia faragha yako, anakudhibiti, mchokonoaji au kukuona huna maana.Lakini...