Monday, December 8, 2014

Kipozi: Uhuru wa habari si upotoshaji



Na Mwandishi Wetu
MKUU wa Wilaya ya Bagamoyo ambaye pia ni mwanahabari, Ahmed Kipozi amesema kuwa uhuru wa vyombo vya habari maana yake si upotoshaji wa habari.
Kipozi ambaye pia ni mtangazaji mkongwe enzi za iliyokuwa redio Tanzania, televisheni ya ITV pamoja na redio Uhuru, alisema hayo katika mkutano mkuu wa Watangazaji kwa mwaka huu, ulioandaliwa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Jijini Dar es Salaam.
Alisema hivi sasa sekta ya habari imekuwa, na kwamba utangazaji unabeba utaifa na uzalendo hivyo lugha zinazotumika kwa miaka ya sasa zimebadilika tofauti na ilivyokuwa zamani.
“Uhuru wa habari maana yake si upotoshaji, lugha, nidhamu ya utangazaji vimebadilika. Ukumbuke kuwa mtangazaji unapotangaza unajibeba mwenyewe pia unabeba taifa,” alisema Kipozi.
Aliongeza kuwa, hivi sasa watangazaji wengi wanaweza kutangaza lakini hawafikishi ujumbe uliokusudiwa tofauti na ilivyokuwa miaka ile ya zamani.
Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Profesa John Nkoma alisema kuwa mabadiliko makubwa ambayo yametokea katika karne hii ni utangazaji wa kutumia teknolojia ya kidijiti.
Na kwamba mfumo huo wa kidijiti umeleta mabadiliko makubwa kwenye maisha ya kila siku kwa sasa unaweza kupata matangazo ya televisheni mahali popote kwa kutumia vifaa mbalimbali kama vile kompyuta, simu za mkononi na kompyuta ndogo za mkononi kwa kupitia mfumo wa intaneti.
Aliongeza kuwa kwa kipindi c ha miaka 20 iliyopita sekta ya utangazaji imekuwa kwa kiwango cha haraka hadi kufikia mwaka huu kuna vituo vya televisheni 28 na redio 94.
mwisho

1 Maoni:

cool wah also browse your site ,
I really like and are excited about this can find your site ..
Greetings Introduction Of My Seo Milanisti
obat perangsang | obat kuat | alat bantu sex

Twitter Facebook