Monday, December 8, 2014

ARU kudahili wanafunzi zaidi ya 7000

Na mwandishi wetu 
Chuo Kikuu Ardhi (ARU) kinatarajia kudahili wanafunzi 7700 ifikapo 2016/17.
Mwenyekiti wa Baraka la Chuo Kiki Ardhi Tabitha Siwale alisema hayo kwenye mahafali ya nane yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. 
Alisema ili mpango huo utekelezwe chuo hakina budi kuongeza idadi ya wahadhiri na wafanyakazi wengine, kupanua miundombinu pamoja na kuongeza vifaa vya kujifunzia na kufundishia. 
"Chuo bado kinakabiliwa na changa moto mbalimbali zikiwemo idadi ya wahadhiri, uchakavu wa miundombinu, upungufu wa vyumba vya miha dhara, maabara, malazi kwa wanafunzi na nyumba za wafanyakazi, "alisema. 
Siwale alisema ili mpango huo utekelezwe zinahitajika shilingi bil 44 katika miaka mitatu ijayo. 
Kwa upande wake Makamu Mkuu Wa ARU, Profesa Idrissa Mshoro alisema kuwa katika mahafali hiyo wanafunzi 964 walihitimu ikilinganishwa na 483 wa mwaka jana. 
Alisema mafanikio hayo yanatokana na ongezeko la udahiliwa wanafunzi ambalo lilianza kukua kwa kasi zaidi mwaka 2010/11. 
Alisema ili kufikia malengo waliojiwekea mwaka wa masomo 2015/16 wanatarajia kuongeza udahili na kufikia 7741. 
Mwisho

0 Maoni:

Twitter Facebook