Friday, December 19, 2008

FAHAMU NJIA SAHIHI YA KUKOSOA ILI MTU ASIKUCHUKIE

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika safu hii inayokujia kila Alhamisi. Ninamshukuru kila mmoja aliyekuwa mstari wa mbele katika kufuatilia mada mbalimbali. Wapo waliotoa ushauri, pongezi, lakini pale nilipokosolewa nilikubali kwani nia ni kuelimisha.Leo tutaangalia mifano mbalimbali katika maisha yetu tunayoweza kuitumia pale tunapotaka kumkosoa mtu yeyote aliyefanya jambo kwa makusudi au kwa kutokujua bila kumfanya ajisikie vibaya.Kwa kuanza, tumuangalie mkurugenzi mmoja aliyekuwa na viwanda mbalimbali vya kutengeneza nguo. Lakini siku moja aliamua kufanya ziara ya ghafla katika kiwanda chake kimoja.Alipofika kiwandani aliwakuta baadhi ya wafanyakazi wake wakivuta sigara karibu kabisa na kibao kinachokataza uvutaji sigara sehemu hiyo.Mkurugenzi huyo akakisogelea kibao hicho na kuwaonyesha wafanyakazi...

NJIA SAHIHI YA KUSHUGHULIKA NA MALALAMIKO

WATU wengi wamejaribu kuwashawishi wengine jinsi wanavyofikiri kufanya kwa kuzungumzia zaidi kuhusu mambo yao. Waache na wengine wazungumze.Kwani wanajua zaidi kuhusu shughuli zao na matatizo kuliko unavyodhani. Kwa hiyo ni vema uendelee kuwauliza maswali ili waweze kukwambia mambo machache wanayoyajua.Watu wengi hujikuta wakiingilia kati pale ambapo hawakubaliani na mazungumzo ya mwingine. Lakini wewe usifanye hivyo. Ni hatari. Hawatakusikiliza wakati bado wana mawazo yao mengi ya kueleza.Hivyo ni vema kusikiliza kwa utulivu na kuweka kumbukumbu kile kinachozungumzwa. Kuwa mtulivu katika hilo. Watie moyo kuelezea mawazo yao yote.Je, unafikiri utaratibu huo ni mzuri? Hebu tumuangalie mfanyabiashara. Kulikuwa na mfanyabiashara moja ambaye alikuwa akitafuta soko kwa ajili ya biashara yake, kabla...

KAMA UMEKOSEA KUBALI KOSA

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika safu hii. Tunamshukuru Mungu kwa kutufikisha tena Alhamisi ya kwanza ya Desemba. Nafikiri kupitia safu hii umepata elimu na maarifa mbalimbali. Leo, tutaangalia jinsi inavyokupasa kukubali kosa endapo utakosea.Katika maisha yetu ya kila siku, ni vema kutambua kuwa unaweza kukosea kwa kufanya jambo makusudi au kwa kutokukusudia. Hivyo basi, endapo utakosea jambo, ni vizuri kukiri kosa pasipo kubisha hiyo ndiyo njia sahihi ya kuishi katika ulimwengu huu.Iwapo umetenda kosa lolote, ukaulizwa na kukiri kukosea, ni rahisi kwa mtu anayekuuliza kuelewa kwamba umetambua kosa lako na kulijutia, hivyo hautarudia tena, tofauti kama ungekataa na kusema hujakosea.Asilimia kubwa ya watu wanapokosea hunyamaza hadi wanapoulizwa. Lakini njia nzuri, unapokosea kujitambua mara...

JARIBU KUWA JASIRI KUKIRI KOSA

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika safu hii ya Maisha Yetu inayokujia kila Alhamisi. Safu hii imekuwa ikielimisha, ikikosoa na hata kutoa muongozo wa maisha ya kila siku.Leo katika safu hii tutaangalia jinsi unavyoweza kujiepusha usiwe na maadui katika maeneo mbalimbali uliyopo. Kuna wakati unaweza kuona umeelemewa na mawazo pasipo kukumbana na tatizo lolote, lakini mtu anapokuambia umekosea, hilo linaweza kukufanya uwe na huzuni katika moyo wako.Hivyo basi, unaweza kumueleza mtu kwamba amekosea kwa kumwangalia, kumwambia au kutumia ishara kama njia ya kumshawishi mtu akuelewe kama vile unavyoweza kuzungumza kwa maneno.Elewa kuwa utapomwambia mtu ana makosa, unafikiri utamfanya akuamini? Hapana. Hiyo si njia sahihi, kwani unaweza kulitatua tatizo hilo kwa busara, maarifa, hekima na staha. Ukitumia...

JINSI UNAVYOWEZA KUJENGA URAFIKI

KILA mmoja hapa duniani ana jukumu la kuwa kiongozi mahali popote alipo - iwe nyumbani, kazini ama shuleni - ili kuwawezesha wengine kufanya kazi kwa kufuata kanuni na sheria zilizopo.Mfano wewe ni kiongozi katika kampuni, shirika au ofisi yoyote, ni jukumu lako kuwaangalia wafanyakazi wenzako kama wanafanyakazi zao kwa kufuata sheria na taratibu za kazi zilizopo.Kama utashindwa kuwasimamia vizuri, ikatokea mmoja wao akapatwa na madhara, jukumu hilo utalibeba wewe kama kiongozi wao. Hivyo basi, kama wewe ni kiongozi katika kampuni ya uhandisi ni vyema kuhakikisha kuwa wafanyakazi unaowasimamia wanatimiza wajibu wao, kwa kuvaa kofia za kufanyia kazi wakati wote wawapo kazini.Inawezekana wakati mwingine wafanyakazi hao wakafanya mazoea na kuacha kuvaa kofia hizo au wakadharau kufuata sheria...

TAFUTA NJIA SAHIHI YA KUTATUA MIGOGORO

JINSI jamii inavyokuwa na mfumo wa aina fulani ya maisha, kuna kila uwezekano wa kujenga mizizi inayoweza kusababisha mikwaruzano mbalimbali.Ni vema kuelewa kuwa, kila jamii ina mfumo wake, hivyo wengine kuona kuwa, hawatendewi haki kama wenzao, hali ambayo itaweza kuchangia kutokuelewana au migongano.Hali hiyo ya kutokuelewana hutokea hasa pale kiongozi wa nchi, wilaya, kijiji, mtaa, kwenye maeneo ya kazi au katika shughuli yoyote inayowashirikisha watu wengi, kiongozi huyo, anaposhindwa kuwawakilisha wote kwa usawa.hali hiyo huwa hutokea kwa kiongozi yeyote ambaye hayuko makini katika utendaji wake, kwani kila mwanadamu ana mahitaji muhimu, hupenda kuwa salama na kutambulika. Sasa basi, ikiwa mahitaji yake hayafikii malengo iliyokusudia, husababisha maamuzi mabovu kutolewa, amani kutoweka...

ZAWADI SI LAZIMA IWE PESA

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika safu hii ya Maisha Yetu kila Alhamisi. Leo tutakwenda kuangalia jinsi unavyoweza kuonyesha zawadi ya upendo kwa watu, hata kama huna fedha.Kila mtu anapenda kupendwa, yakupasa kuwa na rafiki wa karibu atakayekushirikisha katika mambo mbalimbali unayokabiliana nayo.Hivyo ni vema kuwa na rafiki mzuri na kuonyesha upendo wako kwake, kwa sababu wakati mwingine unajikuta hata familia yako inakuwa mbali nawe, hivyo kipindi hicho unakuwa unahitaji mtu wa kuongea naye.Pia ni muhimu kuwa rafiki mzuri kwa sababu unajifunza ni jinsi gani ya kukutana na watu wapya na unajifunza kutokana na makosa yako.Tafuta watu ambao unapenda wawe rafiki zako, kwa kujitambulisha, kumwacha mtu mwingine kukueleza juu ya mambo anayoyapendelea.Mwonyeshe mtu huyo kuwa unamwamini, mwache ajue...

USIIGE FANYA BIASHARA UNAYOIMUDU

HABARI wapenzi wasomaji wetu. Tunamshukuru Mungu kwa siku nyingine ya leo kutuamsha tukiwa wenye afya njema. Kama kawaida leo tutakwenda kuangalia Maisha Yetu ambayo huchapishwa kila Alhamisi.Je, wajua kuwa bahati yako ipo mikononi mwako? Na kama utafanya bidii kwa kutumia mikono yako Mungu aliyokupa ni lazima utaiona.Ninamaanisha kuwa mtu yeyote anayependa mafanikio na kuamua kupambana ili kufikia malengo yake, ni lazima atafanikiwa. Mafanikio hayo yatatokana na jitihada pamoja na bidii anayoionyesha mtu huyo.Mtu yeyote ambaye hatataka kujikwamua kutoka katika hali ya dhiki aliyonayo, atabakia kuwa maskini na tegemezi. Utajiri wa watu wale wanaofanya jitihada na hata kufanikiwa hautamsaidia mtu ambaye hapendi kujishughulisha.Kama hautapenda kujikwamua kutoka katika hali ya dhiki uliyonayo,...

KUJIAMINI KUNASTAWISHA MAISHA YAKO

UTAKUWA na tofauti gani katika maisha yako endapo utakuwa mtu wa kujiamini? Ni nini zaidi utakachokipata? Hilo ni swali ambalo sote tunaweza kujiuliza.Ni ukweli usiopingika, kwamba hali ya kujiamini inasitawisha maisha yako. Hivyo unapokuwa na afya nzuri inakufanya ufikie malengo yako kwa urahisi zaidi.Unapojiamini katika maisha yako na shughuli zako za kila siku, utaweza kuwasaidia na wengine ambao unawasiliana nao katika maeneo mbalimbali iwe ni nyumbani au kazini. Vile vile endapo unakutana na mambo ya kustaajabisha, ya kushtusha au ya mshangao huna haja ya kuogopa, kwa kuwa tayari umeshajijengea hali ya kujiamini, utaikabili hali hiyo kwa urahisi.Ni vizuri kujijengea hali ya kujiamini katika maisha yako kwani watu wote walio na hali hiyo wamekuwa na viwango vya tofauti ambavyo kila moja...

Pages 321234 »
Twitter Facebook