KARIBU mpenzi msomaji katika safu hii ya Maisha Yetu inayokujia kila Alhamisi. Madhumuini makubwa ya safu hii ni kukuelimisha, kukukosoa na kukujenga kiuchumi. Leo utaona ni jinsi marafiki wanavyoweza kuwa kikwazo cha mafanikio yako.Endapo utapata nafasi ya kutulia na kutafakari marafiki ulio nao, utagundua kuwa una nafasi kubwa ya wewe kusimamia mambo yako mwenyewe.Nimeanza kwa kusema hivyo kwa sababu mara nyingine rafiki yako ndiye anayekuwa kikwazo cha mafanikio yako kwa kukurudisha nyuma fikra zako kimaendeleo.Rafiki huyo badala ya kukusaidia kimawazo, atakushawishi muende maeneo ya starehe mara nyingine unapotaka kufanya jambo hukukatisha tamaa kwamba hutafanikiwa na kukutolea mifano ya watu walioshindwa katika maisha yao.Ieleweke wazi kuwa kwenda katika maeneo ya starehe si vibaya, maadamu...