Thursday, February 12, 2009

MARAFIKI WANAWEZA KUWA KIKWAZO CHA MAFANIKIO YAKO

KARIBU mpenzi msomaji katika safu hii ya Maisha Yetu inayokujia kila Alhamisi. Madhumuini makubwa ya safu hii ni kukuelimisha, kukukosoa na kukujenga kiuchumi. Leo utaona ni jinsi marafiki wanavyoweza kuwa kikwazo cha mafanikio yako.Endapo utapata nafasi ya kutulia na kutafakari marafiki ulio nao, utagundua kuwa una nafasi kubwa ya wewe kusimamia mambo yako mwenyewe.Nimeanza kwa kusema hivyo kwa sababu mara nyingine rafiki yako ndiye anayekuwa kikwazo cha mafanikio yako kwa kukurudisha nyuma fikra zako kimaendeleo.Rafiki huyo badala ya kukusaidia kimawazo, atakushawishi muende maeneo ya starehe mara nyingine unapotaka kufanya jambo hukukatisha tamaa kwamba hutafanikiwa na kukutolea mifano ya watu walioshindwa katika maisha yao.Ieleweke wazi kuwa kwenda katika maeneo ya starehe si vibaya, maadamu...

Friday, February 6, 2009

KUFANIKIWA AU KUTOFANIKIWA NI UCHAGUZI WAKO

KARIBUNI wasomaji katika safu hii, leo tutazungumzia kufanikiwa au kushindwa ni uchaguzi wako mwenyewe.Kumbuka umebarikiwa kuwa na uhuru wa maamuzi, kama vile kuchagua aina ya maisha unayotaka kuishi.Kama hivyo sivyo, huwezi kuwa na uwezo wa kutumia vipaji vyako ulivyonavyo.Fahamu kuwa, akili uliyonayo ni nyenzo muhimu ya kukufanya ufanikiwe, kwa kufikiri na kutumia vipaji ulivyo navyo kisha kuvifanyia kazi.Kwa kuwa mafanikio yako yanatokana na akili yako uliyonayo. Endapo utatumia akili, hisia na imani yako kwa busara na kufanyia kazi, ni lazima maisha yako yatakuwa na mabadiliko makubwa ya mafanikio.Una uhuru wa kuchagua namna unavyofikiri, unavyohisi na unavyoamini ili uweze kusonga mbele, kamwe usikubali kuwa na fikra mgando ambazo hazitakusogeza hapo ulipo.Mafanikio au kushindwa kwako...

KILA MTU ANAWEZA KUFANIKIWA

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika siku nyingine ambayo Mwenyezi Mungu ametujalia kuiona. Leo katika safu yetu hii tunaangalia ni jinsi kuweza kufanikiwa.Kumbuka ni juu yako kuchagua kama unataka kufanikiwa, kwani huwezi kupata mafanikio yoyote kwa kuangalia mambo yaliyopita ambayo hayakukuendea vizuri.Ni vema ukimtegemea Mungu pamoja na kuongeza bidii kwa akili na ujuzi aliokupa. Usimtegemee mwanadamu yeyote katika kufanikisha mambo yako kwani atakukatisha tamaa.Kama mwanadamu mwenye akili timamu, una uhuru wa kuchagua jambo unalohitaji. Ni vema ukachagua afya, furaha pamoja na kupata mafanikio. Ili ufanikishe malengo yako ni lazima uwe na mpango na siyo kufanya jambo kwa kubahatisha.Kwani kila mmoja anao uwezo wa kufanikiwa, endapo atakuwa na mipango kamilifu. Kumbuka kila jambo unalolifanya...

Pages 321234 »
Twitter Facebook