Tuesday, January 27, 2009

UKIWEKA NIA UTAFANIKIWA

MIUJIZA inaweza kutokea kwenye maisha yako wakati unapotumia akili katika njia ya kukubali. Na pale unapotambua kwamba kitu pekee kitachokutenganisha kutoka kwenye mafanikio au kushindwa ni vile unavyofikiri, unavyohisi na kuamini.Kama unavyofikiri na kuamini kila saa ya kila siku, unakuwa tayari umeshapanda mbegu ya mafanikio au kushindwa katika mawazo yako.Amini kuwa kufikiri na kuhisi kunakuletea mafanikio. Unaweza kuwa na vipaji vingi vya asili vinavyosubiri kuendelezwa, jitahidi kuvivumbua.Amini kuwa vipaji vyako ni vya thamani na unaweza kuvitimiza kwa kuvifanyia kazi. Amini kushinda mara kwa mara katika vita ya ushindi.Ni bora kuwa na imani ndogo ya kufanya jambo kuliko kukosa kabisa. Huwezi kuwaza mara moja kuwa unataka kuhamia kwenye nyumba mpya bila kufanya maandalizi.Lakini unaweza...

JINSI GANI UNAWEZA KUFANIKIWA - 2

KARIBUNI wapenzi wasomaji kwa siku nyingine tena ya leo, ambayo tutaangalia ni jinsi gani tutaweza kufanikiwa katika maisha yetu. Makala hii ni mwendelezo wa Alhamisi iliyopita katika safu hii ya Maisha Yetu.Kumbuka hukuzaliwa katika dunia hii kuishi au kukabiliana na maisha kwa bahati mbaya. Kila mmoja anajua kuwa maisha ni safari ndefu, mwanzo wa mwanadamu ni kuzaliwa. Na siku yoyote anaweza kufa.Katika maisha tuliyonayo, mwanadamu ana uhuru wa kufanya kile atakacho na kusimamia maisha yake katika jambo alitakalo, kwa nia ya kula matunda mazuri katika maisha. Hivyo mwanadamu anatakiwa kuwa na utayari katika kuyatengeneza maisha yake, ni lazima ajue yeye ni nani na anaelekea wapi.Malengo makubwa ya kiroho ya mwanadamu ni kuwa karibu na Mungu, malengo katika akili ya mwanadamu ni kutambua...

NI JINSI GANI UNAWEZA KUFANIKIWA

UMEZALIWA ili ufanikiwe, mtu yeyote anayekueleza tofauti na hilo, ni mjinga asiyeielewa dunia inavyokwenda.Mafanikio huwafikia wote wanaokubaliana na kanuni, pamoja na sheria zinazokuelekeza kuwa tajiri na kufanikiwa kwenye maisha.Ujuzi huu au ukosefu wa ujuzi ni sababu ya kwanini wengine wanafanikiwa wakati wengine wanashindwa katika maisha.Kanuni hii ya jinsi gani ya mtu anaweza kufanikiwa inamfanya mtu abuni mbinu mbalimbali za kuibua vipaji vipya na kufuata sheria mbalimbali za maendeleo katika akili yake.Ujuzi utakapokua ndiyo silaha yako katika maisha, utakuwa tayari kuyabadili maisha yako. Kama vile mafanikio kutoka kwenye kushindwa, afya kutoka kwenye ugonjwa na furaha kutoka kwenye majonzi.Utawala wa akili yako ni ufunguo wa mafanikio. Kile unachofikiri, kihisi na kukiamini, ndicho...

ARI YA KAZI INAPOKOSEKANA JARIBU NJIA NYINGINE

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika safu hii ya kila Alhamisi. Tunamshukuru Mungu kwa siku hii ambayo tunaukaribisha mwaka mpya wa 2009.Katika safu hii ya Maisha Yetu, tumejifunza kwa mifano mbalimbali kutoka kwa watu walioitumia na kufanikiwa katika maisha yao.Leo, tutamuangalia Chall Wounder, aliyekuwa na meneja katika kiwanda chake ambacho wafanyakazi waligoma kuzalisha, kwa muda kwa kukosa ari ya kufanya kazi.“Mnaendeleaje?” Wounder alimuuliza meneja huyo, ambaye asingeweza kukifanya kiwanda kizalishe kama ilivyotarajiwa, kutokana na mgomo uliokuwepo.“Vizuri,” meneja huyo alijibu. “ Nimejaribu kuwashawishi, kwa viapo vyote bila mafanikio, nimewatishia na kuwaambia kuwa nitawafukuza kazi, lakini vitisho vyote vilikuwa bure. Wameendelea na msimamo wao wa kutokuzalisha,” anasema meneja huyo.Mazungumzo...

Pages 321234 »
Twitter Facebook