
KARIBUNI wapenzi wasomaji katika safu ya ‘Maisha Yetu’. Kwa zaidi ya mwaka sasa nimeandika mambo mbalimbali yanayohusu mafanikio, jinsi ya kuishi na watu mbalimbali, kujua tabia za watu, kujijua mwenyewe na jinsi ya kupambana na maisha katika hali yoyote.Kwa kweli safu yetu imepongezwa sana na tulipokosea tulikubali ushauri kutoka kwa wasomaji wetu. Naamini mtaendelea kutuungana mkono kwa kusoma na kuendelea kutoa ushauri wa kuboresha safu hii.Wiki iliyopita niliishia sehemu inayosema; kumbuka unapoanza kuwa na hofu ya vitu vilivyopita ni kama unajaribu kupanda mazao yako kwenye vumbi.Maana yake ni kwamba yale yaliyopita usiyasumbukie, bali ugange...