Wednesday, July 23, 2008

WAZA MAMBO MAZURI

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika safu ya ‘Maisha Yetu’. Kwa zaidi ya mwaka sasa nimeandika mambo mbalimbali yanayohusu mafanikio, jinsi ya kuishi na watu mbalimbali, kujua tabia za watu, kujijua mwenyewe na jinsi ya kupambana na maisha katika hali yoyote.Kwa kweli safu yetu imepongezwa sana na tulipokosea tulikubali ushauri kutoka kwa wasomaji wetu. Naamini mtaendelea kutuungana mkono kwa kusoma na kuendelea kutoa ushauri wa kuboresha safu hii.Wiki iliyopita niliishia sehemu inayosema; kumbuka unapoanza kuwa na hofu ya vitu vilivyopita ni kama unajaribu kupanda mazao yako kwenye vumbi.Maana yake ni kwamba yale yaliyopita usiyasumbukie, bali ugange...

ONDOA WASIWASI KATIKA MAISHA USONGE MBELE

KARIBUNI wapenzi wasomaji wa safu hii inayowajia kwa lengo la kufundisha na kubadili maisha yetu. Pia safu hii huweza kumtoa mtu katika hali fulani aliyokuwa nayo na kumweka katika hali nyingine.Wiki iliyopita tuliishia sehemu iliyoeleza, unapokuwa kwenye wakati mgumu, kama unaweza kuiondoa hali hiyo ni vizuri, lakini kama huwezi usiipe nafasi moyoni mwako.Endapo utaipa nafasi hali hiyo, itarudisha nyuma maendeleo yako kwa kuwa kila utakapotaka kupiga hatua, hofu ya kufa au kuugua na kuacha mali zako hukujia.Katika vipindi mbalimbali mtu anavyopitia, amekuwa akikutana na hali isiyo nzuri kutokana na mzunguko wa dunia.Hivyo, unapojikuta katika...

KUBALIANA NA HALI USIYOWEZA KUIBADILI

KARIBUNI wapenzi wasomaji katika Safu ya Maisha Yetu, ambayo huelimisha, huadilisha na kubadilisha mambo mbalimbali tunayokabiliana nayo katika maisha yetu ya kila siku.Wiki iliyopita tulimwona Steven baada ya kufiwa na watoto wake wawili mfululizo aliishi kwa hofu na kukata tamaa kwa muda mrefu, lakini siku moja mtoto wake wa kiume (5) alimwomba baba yake amtengenezee boti, ambayo ilimchukua muda mrefu kuimaliza.Kwa maelezo ya Steven, kutengeneza boti hiyo kulichukua muda wa saa tatu, lakini ilipokwisha aligundua muda huo alioutumia katika kazi aliyokuwa akiifanya, uliweza kumpumzisha akili yake na kumpa amani ambayo aliipoteza kwa muda mrefu baada ya kufiwa na watoto wake.Tokea hapo, aligundua kuwa ni vizuri mtu ajishughulishe katika kipindi kigumu anachopitia kama vile kufiwa na mke, mume,...

KUJISHUGHULISHA NI NJIA YA KUONDOA HOFU, WASIWASI

NI vizuri ukakabiliana na hali ya wasiwasi inayokusumbua na kuanza siku mpya. Wasiwasi mara nyingi unasababisha uso wako kuharibika, kukunjika, kupatwa na chunusi, vipele vidogo vidogo, ngozi kukunjamana, nywele kubadilika rangi na wakati mwingine kukatika.Unaweza kuona hali hiyo kuwa ni ya kawaida, lakini sivyo unavyofikiri, hivyo unaweza kukabiliana nayo kwa kuondoa hali hiyo ya hofu na wasiwasi.Je, unapenda maisha? Je, unapenda kuishi maisha marefu na kufurahia afya bora? Unatakiwa kuwa na amani ndani ya moyo wako ambayo itakuwezesha kuishi kwa kujiamini.Tuangalie mfano wa kijana Dave, ambaye alihakikishiwa na daktari wake kuwa ana ugonjwa...

ONDOA WASIWASI ANZA MAISHA MAPYA

MWANAFUNZI aliyekuwa akichukua masomo ya udaktari, alikuwa na wasiwasi wa jinsi ya kufaulu mitihani yake ya mwisho ya kumaliza chuo. Na hata atakapomaliza masomo yake na kufaulu atapelekwa wapi kufanya kazi aliyoisomea na jinsi gani ataweza kumudu maisha.Wakati akitafakari hayo, alijikuta anasoma maneno machache ambayo yalibadilisha mtazamo wake huo, na kumfanya kuwa daktari mmoja maarufu katika kizazi chake, na hata alipofariki kurasa 1,466 ziliandikwa kwa ajili ya kueleza wasifu wake.Maneno hayo ni - “Kazi yetu si kuona kwa upeo mdogo kilicho mbali, bali ni kufanya kile tulichonacho mkononi”.Hata hivyo, mwanafunzi huyo aliamini kuwa njia inayowezekana kuandaa mambo ya kesho ni kufikiri kwa ufahamu wote, pamoja na kuwa na shauku ya kufanya kazi ya leo vizuri zaidi.Aligundua kuwa hiyo ndiyo...

Thursday, July 10, 2008

Bill Gates

Wengine kufikia mfanikio kama aliyo nayo Bill Gates, huona ni ndoto na jambo lisilowezekana, kabisa, lakini amini inawezeka...

Pages 321234 »
Twitter Facebook