ILI ufanikiwe katika biashara yako inakubidi uwe na jitihada za ziada.
Kadiri mtu anavyoongeza jitihada katika usimamizi wa biashara yake, ndivyo anavyopata mafanikio.
Inapaswa kutumia jitihada za kiakili na kimwili.
Watu wengi huanza biashara baada ya kuchoka kutokana na kufanya kazi aliyoajiriwa kwa muda mrefu au kupata ‘presha’ kutoka kwa bosi wake ofisini.
Hivyo fikra kubwa aliyonayo ni kwamba katika biashara yake anakwenda kupumzika kwa kuwa ana wasaidizi, kazi yake itakuwa ni kusaini hundi tu.
Mwisho anakuja kushtukia hakuna biashara inayoendelea kwa kuwa hakuonesha jitihada tokea mwanzo.
Kumbuka kuwa kufanya biashara si jambo rahisi, linahitaji nidhamu ya hali ya juu katika utendaji kazi.
Uanzishwaji na ukuaji wa biashara unahitaji muda mwingi zaidi ya wengi wanavyodhani.
Hapo inabidi...