Thursday, April 4, 2013

Hizi ndizo njia za kufanikiwa kibiashara

ILI ufanikiwe katika biashara yako inakubidi uwe na jitihada za ziada. Kadiri mtu anavyoongeza jitihada katika usimamizi wa biashara yake, ndivyo anavyopata mafanikio. Inapaswa kutumia jitihada za kiakili na kimwili. Watu wengi huanza biashara baada ya kuchoka kutokana na kufanya kazi aliyoajiriwa kwa muda mrefu au kupata ‘presha’ kutoka kwa bosi wake ofisini. Hivyo fikra kubwa aliyonayo ni kwamba katika biashara yake anakwenda kupumzika kwa kuwa ana wasaidizi, kazi yake itakuwa ni kusaini hundi tu. Mwisho anakuja kushtukia hakuna biashara inayoendelea kwa kuwa hakuonesha jitihada tokea mwanzo. Kumbuka kuwa kufanya biashara si jambo rahisi, linahitaji nidhamu ya hali ya juu katika utendaji kazi. Uanzishwaji na ukuaji wa biashara unahitaji muda mwingi zaidi ya wengi wanavyodhani. Hapo inabidi...

Mjasiriamali yeyote anaweza kufanikiwa

WATU wengi wameshindwa kuendelea mbele katika shughuli zao za kijasiriamali kutokana na changamoto wanazokabiliana nazo kibiashara. Lakini ukweli ni kwamba mjasiriamali yeyote anaweza kufanikiwa katika biashara yake kama atafuata sheria na kanuni za kibiashara, ikiwemo kupata mafunzo ya ujasiriamali. Kama unafanya biashara ambayo wateja wanapata huduma wanazohitaji kwa urahisi, ama michezo au sehemu ya kusoma barua pepe zao na kufanya shughuli nyingine zinazohusu mtandao, unakuwa kwenye nafasi ya mafanikio. Lakini kama unapata eneo ambalo silo, utajikuta unafunga haraka biashara hiyo tofauti na matarajio uliyokuwa unayategemea. Biashara nyingi...

Fanya biashara kuendana na wakati uliopo

WIKI iliyopita tuliona ni kwanini biashara inayoanza inashindwa kuingia kwenye ushindani kibiashara, na nini kifanyike ili kukwamua biashara hiyo. Leo tutaangalia sababu nyingine inayokwamisha ama kuyumbisha biashara inayoanza. Ni vema mfanyabiashara yeyote akajua muda wa bidhaa yake aliyonayo imetengenezwa lini na inakwisha lini matumizi yake ili kujua kucheza na soko lake. Endapo umeanzisha biashara na hujafuatilia jambo hilo, inapofikia muda ambao bidhaa hizo zinakwisha muda wake, kwa vyovyote vile utapata hasara kwa kutojiandaa jinsi ya kukabiliana na hali hiyo. vile vile inakupasa kuwapa wateja wako kile wanachokihitaji. hapa ninamaanisha...

Mbinu, kanuni za kufanya biashara

WATU wengi wanapoanza biashara wanakuwa hawafanyi utafiti wa kutosha, matokeo yake biashara wanazozianzisha zinakufa. Hivyo basi, biashara unayoifanya ni vema ukazingatia vitu mbalimbali kabla ya kuifungua, ikiwamo eneo la biashara, samani pamoja na muonekano wake kwa wateja wako. Baadhi ya watu wanaoanza biashara zao wanakuwa na makosa yanayojirudia mara kwa mara kwa kupangisha ofisi za gharama kubwa, kununua samani za bei kubwa pamoja na vifaa mbalimbali, ikiwa ni pamoja na kutoa vipeperushi vya thamani kwa lengo la kuujulisha umma kuhusu biashara hiyo, bila kuangalia bajeti aliyojiwekea kwa biashara hiyo. Lakini ni vema kujua mbinu na kanuni za kufanya biashara ili uweze kusonga mbele badala ya kurudi nyuma, ama kuifunga baada ya muda mfupi. Mara nyingi wateja wanapenda kufanya biashara...

Acha mawazo hasi

KATIKA makala zangu za Maisha Yetu niliwahi kuandika kwamba njia pekee ya kufanikiwa ni kutoruhusu mawazo yanayoleta kizuizi, kama vile kuwaza umaskini, kuwa na hofu au wasiwasi kila mara kwa kile unachokifanya. Endapo wewe ni mtu wa aina hiyo inakupasa ubadilike ili usonge mbele kimafanikio. Mara tu unapomaliza kuyachuja mawazo yako, unachagua yale unayotaka kuyafanyia kazi. Utagundua kuwa nayo yanahitaji kuongezewa ubora wake. Jifunze kutokufunga milango yako ya kuwa mbunifu. Ni jambo lisilowezekana kati yetu kuwa kinyume cha ujuzi tulionao. Mfano mtu hawezi kupita mbele ya gari liendalo kasi kwa kuwa anajua kuwa ataumia, hawezi kuogelea...

Kufikiri kunaleta mafanikio

KWA mara nyingine nakukaribisha katika safu ya Maisha Yetu, ili uweze kujifunza mambo yaliyopo, yanayotokea na yanayoendelea kutokea katika dunia hii. Miujiza inaweza kutokea kwenye maisha yako wakati unapotumia akili katika njia ya kukubali. Na pale unapotambua kwamba kitu pekee kitachokutenganisha kutoka kwenye mafanikio au kushindwa ni vile unavyofikiri, unavyohisi na kuamini. Kama unavyofikiri na kuamini kila siku, unakuwa tayari umeshapanda mbegu ya mafanikio au kushindwa katika mawazo yako. Amini kuwa kufikiri na kuhisi kunakuletea mafanikio. Unaweza kuwa na vipaji vingi vya asili vinavyosubiri kuendelezwa, jitahidi kuvivumbua. Amini...

JINSI YA KUEPUKA KUPATA HASARA

KATIKA biashara yako hali inapokwenda mrama ni vema kuweka tamko la kusitisha hasara uliyoipata, kwamba hauko tayari kukubali hasara hiyo iendelee. Jitahidi kuweka mikakati zaidi ya kuiboresha biashara yako na kuomba ushauri wa kimaendeleo kwa wafanyabiashara waliofanikiwa. Tumwangalie mfanyabiashara John Robert, aliyekuwa amepewa fedha na rafiki zake kiasi cha dola 200,000 za Kimarekani, ili kuwekeza katika soko la hisa. Baada ya kupewa fedha hizo na kuzifanyia biashara, Robert alifikiri kuwa angepata faida ambayo ingemfanya awe na maendeleo zaidi katika maisha yake, lakini kwa bahati mbaya ilikuwa kinyume na matarajio yake. Awali, alipoanza biashara hiyo alipata faida iliyomfanya asiwe mbunifu katika biashara yake, lakini matokeo yake ni kwamba baada ya muda mfupi alifilisika. Mfanyabiashara...

Wednesday, April 3, 2013

UKOSEFU WA MAWAZO HUUA BIASHARA

KILA siku mamilioni ya watu wamekuwa wakikabiliana na changamoto mbalimbali katika dunia hii tunayoishi. Mbali na misukosuko katika ndoa au mahusiano ya mwanamke na mwanamme, hali inayochangia kutokuelewana, msongo wa mawazo, ugonjwa, wengine hufikia hatua ya kujinyonga. Kadhia nyingine kubwa ni kuhusu kushindwa au kufilisika kwa biashara aliyonayo. Kutokufanikiwa kwa biashara hizo kunatokana na mipango katika biashara, masoko na suala la kifedha. Pia inakuwa si rahisi kujua kwa undani ni kwanini biashara ndogo zinakufa. Haitoshi kusema kuwa ni kutokana na ushindani wa kibiashara uliopo, ama mabadiliko ya teknolojia, madeni, mauzo madogo, ama...

Pages 321234 »
Twitter Facebook