Monday, December 8, 2014

Chuo Kikuu chatoa zawadi kwa wanafunzi

Na Mwandishi Wetu
CHUO Kikuu Ardhi (ARU) kimewazawadia wanafuzi 130 wa masomo mbalimbali zawadi zenye thamani ya zaidi ya shilingi mil. 60 kutokana na ufaulu mzuri katika masomo yao.
Zawadi hizo ni fedha taslimu, mashine za upimaji ardhi na laptop katika hafla fupi iliyofanyika chuoni hapo Jijini Dar es Salaam.
Akikabidhi zawadi hizo, Makamu Mkuu wa chuo hicho Idrissa Mshoro alisema kuwa wanafunzi wa kike wameendelea kufanya vizuri katika masomo yao ambapo wamefikia wastani wa asilimia 40 dhidi ya asilimia 30 kwa wanaume.
Alisema miongoni mwa wanafunzi waliopata zawadi hizo hawakuwa na sifa za kujiunga katika chuo hicho mpaka walipopewa kozi fupi ambapo baada ya usaili walifaulu.
Profesa Mshoro alisema kuwa waliamua kuwa na mfumo huo baada ya kuona wanafunzi wengi wanataka kujiunga na chuo hicho kwa ajili ya elimu ya juu lakini alama zao walizopata katika shule walizokuwa wanasoma haziwawezesha kujiunga.
Kwa upande wake Makamu Mkuu wa Taaluma chuoni hapo, Gabriel Kassenga alisema kuwa matokeo ya mwaka huu yameendelea kufuta dhana kuwa wanawake sio wazuri katika masomo ya sayansi.
“Wameonyesha uwezo mkubwa kwa kutwaa zawadi nyingi kuliko wanaume na hiyo ni dalili kuwa sayansi sio ya wanaume pekee” aisema na kuongeza kuwa hata mwaka jana wanawake waliongoza kwa kupata tuzo nyingi za kitaaluma kuliko wanaume.
Mwisho………………

ARU kudahili wanafunzi zaidi ya 7000

Na mwandishi wetu 
Chuo Kikuu Ardhi (ARU) kinatarajia kudahili wanafunzi 7700 ifikapo 2016/17.
Mwenyekiti wa Baraka la Chuo Kiki Ardhi Tabitha Siwale alisema hayo kwenye mahafali ya nane yaliyofanyika jijini Dar es Salaam. 
Alisema ili mpango huo utekelezwe chuo hakina budi kuongeza idadi ya wahadhiri na wafanyakazi wengine, kupanua miundombinu pamoja na kuongeza vifaa vya kujifunzia na kufundishia. 
"Chuo bado kinakabiliwa na changa moto mbalimbali zikiwemo idadi ya wahadhiri, uchakavu wa miundombinu, upungufu wa vyumba vya miha dhara, maabara, malazi kwa wanafunzi na nyumba za wafanyakazi, "alisema. 
Siwale alisema ili mpango huo utekelezwe zinahitajika shilingi bil 44 katika miaka mitatu ijayo. 
Kwa upande wake Makamu Mkuu Wa ARU, Profesa Idrissa Mshoro alisema kuwa katika mahafali hiyo wanafunzi 964 walihitimu ikilinganishwa na 483 wa mwaka jana. 
Alisema mafanikio hayo yanatokana na ongezeko la udahiliwa wanafunzi ambalo lilianza kukua kwa kasi zaidi mwaka 2010/11. 
Alisema ili kufikia malengo waliojiwekea mwaka wa masomo 2015/16 wanatarajia kuongeza udahili na kufikia 7741. 
Mwisho

NHC kutatua matatizo ya wananchi



Na Mwandishi Wetu
MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Nyumba  nchini (NHC), Nehemia Mchechu, amesema kuwa wanaiangalia miradi waliyonayo ni jinsi gani inaweza kutatua matatizo waliyonayo wananchi.
Mchechu alisema hayo jjijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza katika mjadala ulioandaliwa na Chuo Kikuu Ardhi (ARU), wakati akiwasilisha mada yake.
Alisema NHC inaangalia ni jinsi gani watengeneze vitovu vya miji ambavyo kutakuwa na makazi ya watu, biashara mbalimbali pamoja na ofisi ili kumpunguzia mwananchi usumbufu wa kutembea muda mrefu.
“Je NHC katika miradi yao wanafanya nini ili wananchi waishi vizuri? Tunachoangalia miradi yetu tuliyonayo ni jinsi gani inaweza kutatua matatizo na kurahisisha huduma kwa wananchi,” alisema Mchechu.
Mchechu alisema kuna miradi Kawe ‘apartment’ iliyopo Dar es Salaam ambayo itawezesha watu kupata mahitaji yote kwa pamoja.
“Ukimfanya mtu akaishi na kufanya kazi karibu na ofisi, ataongeza kipato na kupunguza matumizi kwa kuwa hatasafiri tena mwendo mrefu kwa ajili ya kuwahi kazini, pia itafanya awe na afya bora kwa kupunguza msongo unaotokana na foleni,” alisema Mkurugenzi huyo.
Naye Profesa Lusugga Kironde ambaye anashughulika na masuala ya Maendeleo ya Ardhi na Uthamini (ARU),alisema kuwa siku hizi watu wanakuja mjini kuishi siyo kuondoka tofauti na zamani, hivyo wanaangalia masuala ya kazi, makazi na jinsi wanavyojitambua ili kuwezesha waishi vizuri.
Pia alishangazwa na kitendo cha kuvunja majengo ya zamani na kuwekwa mapya kwa kuwa kinadhoofisha fursa za utalii.
mwisho



 NHC kupunguza matatizo ya wananchi

Na Mwandishi Wetu
MKURUGENZI Mkuu wa Shirika la Nyumba  nchini (NHC), Nehemia Mchechu, amesema kuwa wanaiangalia miradi waliyonayo ni jinsi gani inaweza kutatua matatizo waliyonayo wananchi.
Mchechu alisema hayo jjijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza katika mjadala ulioandaliwa na Chuo Kikuu Ardhi (ARU), wakati akiwasilisha mada yake.
Alisema NHC inaangalia ni jinsi gani watengeneze vitovu vya miji ambavyo kutakuwa na makazi ya watu, biashara mbalimbali pamoja na ofisi ili kumpunguzia mwananchi usumbufu wa kutembea muda mrefu.
“Je NHC katika miradi yao wanafanya nini ili wananchi waishi vizuri? Tunachoangalia miradi yetu tuliyonayo ni jinsi gani inaweza kutatua matatizo na kurahisisha huduma kwa wananchi,” alisema Mchechu.
Mchechu alisema kuna miradi Kawe ‘apartment’ iliyopo Dar es Salaam ambayo itawezesha watu kupata mahitaji yote kwa pamoja.
“Ukimfanya mtu akaishi na kufanya kazi karibu na ofisi, ataongeza kipato na kupunguza matumizi kwa kuwa hatasafiri tena mwendo mrefu kwa ajili ya kuwahi kazini, pia itafanya awe na afya bora kwa kupunguza msongo unaotokana na foleni,” alisema Mkurugenzi huyo.
Naye Profesa Lusugga Kironde ambaye anashughulika na masuala ya Maendeleo ya Ardhi na Uthamini (ARU),alisema kuwa siku hizi watu wanakuja mjini kuishi siyo kuondoka tofauti na zamani, hivyo wanaangalia masuala ya kazi, makazi na jinsi wanavyojitambua ili kuwezesha waishi vizuri.
Pia alishangazwa na kitendo cha kuvunja majengo ya zamani na kuwekwa mapya kwa kuwa kinadhoofisha fursa za utalii.
mwisho

Tuesday, October 28, 2014

TCRA KUTOA MWONGOZO KWA WATANGAZAJI KWENYE UCHAGUZI


MAMLAKA ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imeandaa rasimu ya mwongozo utakaofuatwa na vituo vya utangazaji katika kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa, wabunge na raisi lengo likiwa kuweka usawa na uwazi katika kipindi cha uchaguzi, wakati wa uchaguzi na baada ya uchaguzi kufanyika.
Mwenyekiti wa Kamati ya Maudhui ya mamlaka hiyo Margaret Munyagi alisema hayo katika mkutano wa kupokea maoni ya wadau juu ya utaratibu wa kuandaa na kurusha vipindi vinavyohusu vyama vya siasa wakati wa uchaguzi.
Alisema kuingia kwa mfumo wa vyama vingi vya siasa nchini 1993, kulienda sambamba na kuanzishwa kwa vituo binafsi vya utangazaji, hivyo ongezeko la vituo hivyo limekuwa ni kichocheo cha kukuza demokrasia, kuboresha amani, kudumisha umoja na mshikamano wa taifa.
“Kama mnavyojua nchi yetu inategemea kuingia kwenye kipindi cha uchaguzi wa serikali za mitaa, wabunge na rais ifikapo 2015. Uchaguzi ni mchakato muhimu sana katika kukuza na kuimarisha demokrasia ya n chi husika,” alisema.
Munyagi alisema kuwa, vipindi vinavyotangaza masuala ya uchaguzi vinahitaji umakini mkubwa pamoja na uwepo wa mizani katika muda wanaopewa vyama vya siasa, kuwepo kwa uwazi, kufuata sheria na kanuni husika.
Alisisitiza kuwa, kukamilika kwa mwongozo huo kutawasaidia watangazaji na waandaaji wa vipindi kuepuka kufanya makosa ambayo kama yasipodhibitiwa yanaweza kusababisha uchochezi na kuleta mifarakano miongoni mwa jamii.
Alisema, tofauti na mategemeo hayo baadhi ya vyombo vya utangazaji vimekuwa vikikiuka sheria na kanuni kwa kuwa maudhui yanayotangazwa hayazingatii maadili ya kitanzania badala yake vimechangia kuharibu utamaduni wetu.
Pia vingine vimesahau madhumuni ya kuanzishwa kwao na wajibu wao katika jamii, hivyo kujiingiza katika masuala ya uchochezi pamoja na uvunjifu wa amani na utulivu.
Awali Mkurugenzi wa Utangazaji TCRA, Habbi Gunze alisema kuwa mpaka sasa kuna vituo vya redio 95, pamoja na  vya televisheni 28 nchini, hivyo ni bora vikapata mwongozo maalum wa namna ya kuandika habari za uchaguzi.


mwisho

Twitter Facebook